[1] BWANA anatawala, nchi na ifurahi, visiwa vyote vishangilie. [2] Mawingu na giza nene vinamzunguka, haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake cha enzi. [3] Moto hutangulia mbele zake na huteketeza adui zake pande zote. [4] Umeme wake wa radi humulika dunia, nchi huona na kutetemeka. [5] Milima huyeyuka kama nta mbele za BWANA, mbele za Bwana wa dunia yote. [6] Mbingu zinatangaza haki yake, na mataifa yote huona utukufu wake. [7] Wote waabuduo sanamu waaibishwa, wale wajisifiao sanamu: mwabuduni yeye, enyi miungu yote! [8] Sayuni husikia na kushangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako, Ee BWANA. [9] Kwa kuwa wewe, Ee BWANA, ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote; umetukuka sana juu ya miungu yote. [10] Wale wanaompenda BWANA na wauchukie uovu, kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu. [11] Nuru huangaza wenye haki na furaha kwa watu wanyofu wa moyo. [12] Furahini katika BWANA, ninyi mlio wenye haki, lisifuni jina lake takatifu.