[1] Njooni, tumwimbie BWANA kwa furaha; tumfanyie kelele za shangwe Mwamba wa wokovu wetu. [2] Tuje mbele zake kwa shukrani, tumtukuze kwa vinanda na nyimbo. [3] Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu, mfalme mkuu juu ya miungu yote. [4] Mkononi mwake mna vilindi vya dunia, na vilele vya milima ni mali yake. [5] Bahari ni yake, kwani ndiye aliifanya, na mikono yake iliumba nchi kavu. [6] Njooni, tusujudu, tumwabudu, tupige magoti mbele za BWANA Muumba wetu, [7] kwa maana yeye ndiye Mungu wetu, na sisi ni watu wa malisho yake, kondoo chini ya utunzaji wake. Kama mkiisikia sauti yake leo, [8] msiifanye mioyo yenu migumu kama mlivyofanya kule Meriba, kama mlivyofanya siku ile kule Masa jangwani, [9] ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu. [10] Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile, nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka, nao hawajazijua njia zangu.” [11] Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu, “Kamwe hawataingia rahani mwangu.”