Zaburi 94:1-23 ONEN

[1] Ee BWANA, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa. [2] Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili. [3] Hata lini, waovu, Ee BWANA, hata lini waovu watashangilia? [4] Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno. [5] Ee BWANA, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako. [6] Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima. [7] Nao husema, “BWANA haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.” [8] Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima? [9] Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione? [10] Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa? [11] BWANA anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili. [12] Ee BWANA, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako, [13] unampa utulivu siku za shida, mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya mwovu. [14] Kwa kuwa BWANA hatawakataa watu wake, hatauacha urithi wake. [15] Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, wote walio na mioyo minyofu wataifuata. [16] Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu? Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu? [17] Kama BWANA asingelinisaidia upesi, ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo. [18] Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” Ee BWANA, upendo wako ulinishikilia. [19] Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu. [20] Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe, ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake? [21] Huungana kuwashambulia wenye haki, kuwahukumu kufa wasio na hatia. [22] Lakini BWANA amekuwa ngome yangu, na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia. [23] Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; BWANA Mungu wetu atawaangamiza.

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.