[1] Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli. [2] Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni. [3] Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita. [4] Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori. [5] Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake. [6] Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya. [7] Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika? [8] Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya: [9] wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi. [10] Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi. [11] Wekeni nadhiri kwa BWANA Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa. [12] Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.