[1] Ee Mungu, tunakushukuru, tunakushukuru wewe, kwa kuwa jina lako li karibu; watu husimulia matendo yako ya ajabu. [2] Unasema, “Ninachagua wakati maalum; ni mimi nihukumuye kwa haki. [3] Wakati dunia na watu wake wote inapotetemeka, ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara. [4] Kwa wale wenye majivuno ninasema, ‘Msijisifu tena,’ kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu. [5] Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu; msiseme kwa shingo zilizonyooshwa.’ ” [6] Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu. [7] Bali Mungu ndiye ahukumuye: Humshusha huyu na kumkweza mwingine. [8] Mkononi mwa BWANA kuna kikombe kilichojaa mvinyo unaotoka povu uliochanganywa na vikolezo; huumimina, nao waovu wote wa dunia hunywa mpaka tone la mwisho. [9] Bali mimi, nitatangaza hili milele; nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo. [10] Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote, bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.