Zaburi 70:1-5 ONEN

[1] Ee Mungu, ufanye haraka kuniokoa; Ee BWANA, njoo hima unisaidie. [2] Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu. [3] Wale waniambiao, “Aha! Aha!” warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao. [4] Lakini wote wakutafutao washangilie na kukufurahia, wale wapendao wokovu wako siku zote waseme, “Mungu na atukuzwe!” [5] Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji; Ee Mungu, unijie haraka. Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu; Ee BWANA, usikawie.

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.