[1] Ee Mungu, unisikie ninapoeleza lalamiko langu, uyahifadhi maisha yangu kutokana na vitisho vya adui. [2] Unifiche kutokana na shauri la siri la waovu, kutokana na zile kelele za kundi la watenda mabaya. [3] Wananoa ndimi zao kama panga na kuelekeza maneno yao kama mishale ya kufisha. [4] Hurusha mishale kutoka kwenye mavizio kwa mtu asiye na hatia, humrushia ghafula bila woga. [5] Kila mmoja humtia moyo mwenzake katika mipango mibaya; huzungumza juu ya kuficha mitego yao, nao husema, “Ni nani ataiona?” [6] Hufanya shauri baya la dhuluma na kusema, “Tumebuni mpango mkamilifu!” Hakika nia na moyo wa mwanadamu vina hila. [7] Bali Mungu atawapiga kwa mishale, nao ghafula wataangushwa. [8] Atageuza ndimi zao wenyewe dhidi yao na kuwaleta kwenye maangamizi; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao kwa dharau. [9] Wanadamu wote wataogopa, watatangaza kazi za Mungu na kutafakari yale aliyoyatenda. [10] Wenye haki na wafurahi katika BWANA, na wakimbilie kwake; wanyofu wote wa moyo na wamsifu yeye!