[1] Ee BWANA, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako. [2] Unirehemu BWANA, kwa maana nimedhoofika; Ee BWANA, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali. [3] Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee BWANA, mpaka lini? [4] Geuka Ee BWANA, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako. [5] Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? [6] Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi. [7] Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote. [8] Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana BWANA amesikia kulia kwangu. [9] BWANA amesikia kilio changu kwa huruma, BWANA amekubali sala yangu. [10] Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.