Zaburi 47:1-9 ONEN

[1] Pigeni makofi, enyi mataifa yote, mpigieni Mungu kelele za shangwe! [2] Jinsi gani alivyo wa kutisha, BWANA Aliye Juu Sana, Mfalme mkuu juu ya dunia yote! [3] Ametiisha mataifa chini yetu watu wengi chini ya miguu yetu. [4] Alituchagulia urithi wetu, fahari ya Yakobo, aliyempenda. [5] Mungu amepaa kwa kelele za shangwe, BWANA kwa sauti za tarumbeta. [6] Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa, mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa. [7] Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote, mwimbieni zaburi za sifa. [8] Mungu anatawala juu ya mataifa, Mungu ameketi juu ya kiti chake cha enzi kitakatifu. [9] Wakuu wa mataifa wanakusanyika kama watu wa Mungu wa Abrahamu, kwa kuwa wafalme wa dunia ni mali ya Mungu; yeye ametukuka sana.

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.