[1] Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. [2] Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari. [3] Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake. [4] Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi. [5] Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema. [6] Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka. [7] BWANA Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu. [8] Njooni mkaone kazi za BWANA jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. [9] Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto. [10] “Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.” [11] BWANA Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.