[1] Nitakutukuza wewe, Ee BWANA, kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, na hukuacha adui zangu washangilie juu yangu. [2] Ee BWANA, Mungu wangu, nilikuita unisaidie na wewe umeniponya. [3] Ee BWANA, umenitoa Kuzimu, umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. [4] Mwimbieni BWANA, enyi watakatifu wake; lisifuni jina lake takatifu. [5] Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, bali upendo wake hudumu siku zote. Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, lakini asubuhi kukawa na furaha. [6] Nilipofanikiwa nilisema, “Sitatikiswa kamwe.” [7] Ee BWANA, uliponijalia, uliuimarisha mlima wangu, lakini ulipouficha uso wako nilifadhaika. [8] Kwako wewe, Ee BWANA, niliita, kwa Bwana niliomba rehema: [9] “Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? Katika kushuka kwangu shimoni? Je, mavumbi yatakusifu? Je, yatatangaza uaminifu wako? [10] Ee BWANA, unisikie na kunihurumia, Ee BWANA, uwe msaada wangu.” [11] Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe, [12] ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. Ee BWANA Mungu wangu, nitakushukuru milele.