Zaburi 20:1-9 ONEN

[1] BWANA na akujibu unapokuwa katika dhiki, jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako. [2] Na akutumie msaada kutoka patakatifu na akupatie msaada kutoka Sayuni. [3] Na azikumbuke dhabihu zako zote, na azikubali sadaka zako za kuteketezwa. [4] Na akujalie haja ya moyo wako, na aifanikishe mipango yako yote. [5] Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda, tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu. BWANA na akupe haja zako zote. [6] Sasa nafahamu kuwa BWANA humwokoa mpakwa mafuta wake, humjibu kutoka mbingu yake takatifu kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume. [7] Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi, bali sisi tutalitumainia jina la BWANA, Mungu wetu. [8] Wao wameshushwa chini na kuanguka, bali sisi tunainuka na kusimama imara. [9] Ee BWANA, mwokoe mfalme! Tujibu tunapokuita!

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.