[1] Msifuni BWANA! Ee nafsi yangu, umsifu BWANA, [2] Nitamsifu BWANA maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu sifa wakati wote niishipo. [3] Usiweke tumaini lako kwa wakuu, kwa wanadamu ambao hufa, ambao hawawezi kuokoa. [4] Roho yao itokapo hurudi mavumbini, siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma. [5] Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake ni katika BWANA, Mungu wake, [6] Muumba wa mbingu na nchi, na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: BWANA anayedumu kuwa mwaminifu milele na milele. [7] Naye huwapatia haki walioonewa na kuwapa wenye njaa chakula. BWANA huwaweka wafungwa huru, [8] BWANA huwafumbua vipofu macho, BWANA huwainua waliolemewa na mizigo yao, BWANA huwapenda wenye haki. [9] BWANA huwalinda wageni na kuwategemeza yatima na wajane, lakini hupinga njia za waovu. [10] BWANA atamiliki milele, Mungu wako, ee Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni BWANA.