[1] Mshukuruni BWANA, kwa kuwa ni mwema. Fadhili zake zadumu milele. [2] Mshukuruni Mungu wa miungu. Fadhili zake zadumu milele. [3] Mshukuruni Bwana wa mabwana: Fadhili zake zadumu milele. [4] Kwake yeye pekee atendaye maajabu makuu, Fadhili zake zadumu milele. [5] Ambaye kwa ufahamu wake aliziumba mbingu, Fadhili zake zadumu milele. [6] Ambaye aliitandaza dunia juu ya maji, Fadhili zake zadumu milele. [7] Ambaye aliumba mianga mikubwa, Fadhili zake zadumu milele. [8] Jua litawale mchana, Fadhili zake zadumu milele. [9] Mwezi na nyota vitawale usiku, Fadhili zake zadumu milele. [10] Kwake yeye aliyemuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, Fadhili zake zadumu milele. [11] Na kuwatoa Israeli katikati yao, Fadhili zake zadumu milele. [12] Kwa mkono wenye nguvu ulionyooshwa, Fadhili zake zadumu milele. [13] Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu, Fadhili zake zadumu milele. [14] Na kuwapitisha Israeli katikati yake, Fadhili zake zadumu milele. [15] Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu, Fadhili zake zadumu milele. [16] Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa, Fadhili zake zadumu milele. [17] Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu, Fadhili zake zadumu milele. [18] Naye aliwaua wafalme wenye nguvu, Fadhili zake zadumu milele. [19] Sihoni mfalme wa Waamori, Fadhili zake zadumu milele. [20] Ogu mfalme wa Bashani, Fadhili zake zadumu milele. [21] Akatoa nchi yao kuwa urithi, Fadhili zake zadumu milele. [22] Urithi kwa Israeli mtumishi wake, Fadhili zake zadumu milele. [23] Aliyetukumbuka katika unyonge wetu, Fadhili zake zadumu milele. [24] Alituweka huru toka adui zetu, Fadhili zake zadumu milele. [25] Ambaye humpa chakula kila kiumbe. Fadhili zake zadumu milele. [26] Mshukuruni Mungu wa mbinguni, Fadhili zake zadumu milele.