Zaburi 128:1-6 ONEN

[1] Heri ni wale wote wamchao BWANA, waendao katika njia zake. [2] Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako. [3] Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako. [4] Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye BWANA. [5] BWANA na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu, [6] nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.