Zaburi 129:1-8 ONEN

[1] Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa: [2] wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda. [3] Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu. [4] Lakini BWANA ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu. [5] Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu. [6] Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua; [7] kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake. [8] Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya BWANA iwe juu yako; tunakubariki katika jina la BWANA.”

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.