Zaburi 127:1-5 ONEN

[1] BWANA asipoijenga nyumba, wajengao hufanya kazi bure. BWANA asipoulinda mji, walinzi wakesha bure. [2] Mnajisumbua bure kuamka mapema na kuchelewa kulala, mkitaabikia chakula: kwa maana yeye huwapa usingizi wapenzi wake. [3] Wana ni urithi utokao kwa BWANA, watoto ni zawadi kutoka kwake. [4] Kama mishale mikononi mwa shujaa ndivyo walivyo wana awazaao mtu katika ujana wake. [5] Heri mtu ambaye podo lake limejazwa nao. Hawataaibishwa wanaposhindana na adui zao langoni.

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.