[1] BWANA anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike. [2] BWANA ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote. [3] Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu! [4] Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa. [5] Mtukuzeni BWANA Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu. [6] Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita BWANA, naye aliwajibu. [7] Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa. [8] Ee BWANA, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya. [9] Mtukuzeni BWANA Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana BWANA Mungu wetu ni mtakatifu.