Zaburi 150:1-6 ONEN

[1] Msifuni BWANA. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu. [2] Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake. [3] Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze, [4] msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi, [5] msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana. [6] Kila chenye pumzi na kimsifu BWANA. Msifuni BWANA!

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.