Zaburi 120:1-7 ONEN

[1] Katika dhiki yangu namwita BWANA, naye hunijibu. [2] Ee BWANA, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu. [3] Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu? [4] Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu. [5] Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari! [6] Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani. [7] Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.