Zaburi 11:1-7 ONEN

[1] Kwa BWANA ninakimbilia, unawezaje basi kuniambia: “Ruka kama ndege kwenye mlima wako. [2] Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao, huweka mishale kwenye uzi wake, wakiwa gizani ili kuwapiga wale wanyofu wa moyo. [3] Wakati misingi imeharibiwa, mwenye haki anaweza kufanya nini?” [4] BWANA yuko ndani ya Hekalu lake takatifu; BWANA yuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni. Huwaangalia wana wa watu, macho yake yanawajaribu. [5] BWANA huwajaribu wenye haki, lakini waovu na wanaopenda jeuri, nafsi yake huwachukia. [6] Atawanyeshea waovu makaa ya moto mkali na kiberiti kinachowaka, upepo wenye joto kali ndio fungu lao. [7] Kwa kuwa BWANA ni mwenye haki, yeye hupenda haki. Wanyofu watauona uso wake.

About this translation

Life Bible app icon
Get the Life Bible app Read offline, sync highlights and notes, and study with your library on any device.