Mwanzo 5:1-32 ONEN
[1] Hii ni orodha iliyoandikwa ya vizazi vya Adamu. Wakati Mungu alipomuumba Adamu, alimfanya kwa sura ya Mungu. [2] Aliwaumba mwanaume na mwanamke, akawabariki. Walipokwisha kuumbwa, akawaita “mwanadamu.” [3] Adamu alipokuwa ameishi miaka 130, alikuwa na mwana aliyekuwa na sura yake, mwenye kufanana naye. Akamwita Sethi. [4] Baada ya Sethi kuzaliwa, Adamu aliishi miaka 800, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [5] Adamu aliishi jumla ya miaka 930, ndipo akafa. [6] Sethi alipokuwa ameishi miaka 105, akamzaa Enoshi. [7] Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [8] Sethi aliishi jumla ya miaka 912, ndipo akafa. [9] Enoshi alipokuwa ameishi miaka tisini, akamzaa Kenani. [10] Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815, naye alikuwa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [11] Enoshi aliishi jumla ya miaka 905, ndipo akafa. [12] Kenani alipokuwa ameishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli. [13] Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [14] Kenani aliishi jumla ya miaka 910, ndipo akafa. [15] Mahalaleli alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi. [16] Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [17] Mahalaleli aliishi jumla ya miaka 895, ndipo akafa. [18] Yaredi alipokuwa ameishi miaka 162, akamzaa Enoki. [19] Baada ya kumzaa Enoki, Yaredi aliishi miaka 800, naye akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [20] Yaredi aliishi jumla ya miaka 962, ndipo akafa. [21] Enoki alipokuwa ameishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. [22] Baada ya kumzaa Methusela, Enoki alitembea na Mungu miaka 300, na akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [23] Enoki aliishi jumla ya miaka 365. [24] Enoki akatembea na Mungu, kisha akatoweka, kwa sababu Mungu alimchukua. [25] Methusela alipokuwa ameishi miaka 187, akamzaa Lameki. [26] Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [27] Methusela aliishi jumla ya miaka 969, ndipo akafa. [28] Lameki alipokuwa ameishi miaka 182, alimzaa mwana. [29] Akamwita jina lake Noa, akasema, “Yeye ndiye atakayetufariji katika kazi na maumivu makali ya mikono yetu yaliyosababishwa na ardhi iliyolaaniwa na BWANA.” [30] Baada ya Noa kuzaliwa, Lameki aliishi miaka 595, akawa na watoto wengine wa kiume na wa kike. [31] Lameki aliishi jumla ya miaka 777, ndipo akafa. [32] Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.
