1 Nyakati 2:1-55 ONEN
[1] Hawa ndio waliokuwa wana wa Israeli: Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Zabuloni, [2] Dani, Yosefu, Benyamini, Naftali, Gadi na Asheri. [3] Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa BWANA, kwa hiyo BWANA alimuua. [4] Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano. [5] Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli. [6] Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano. [7] Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu. [8] Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya. [9] Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu. [10] Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda. [11] Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi, [12] Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese. [13] Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea, [14] wa nne Nethaneli, wa tano Radai, [15] wa sita Osemu, na wa saba Daudi. [16] Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli. [17] Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli. [18] Kalebu mwana wa Hesroni akazaa wana na mkewe Azuba (na pia na Yeriothi). Hawa ndio wana Azuba aliomzalia Kalebu: Yesheri, Shobabu na Ardoni. [19] Azuba alipofariki, Kalebu akamwoa Efrathi, ambaye alimzalia Huri. [20] Huri akamzaa Uri, Uri akamzaa Bezaleli. [21] Hatimaye, Hesroni akakutana kimwili na binti wa Makiri babaye Gileadi (ambaye alimwoa alipokuwa na umri wa miaka sitini), naye akamzaa Segubu. [22] Segubu akamzaa Yairi, ambaye alitawala miji ishirini na mitatu katika Gileadi. [23] (Lakini Geshuri na Aramu wakateka miji ya Hawoth-Yairi, pamoja na Kenathi na viunga vyake; jumla ilikuwa miji sitini.) Wote hawa walikuwa wazao wa Makiri babaye Gileadi. [24] Baada ya Hesroni kufa huko Efrathi, Abiya mjane wa Hesroni akamzalia Ashuru, aliye baba wa Tekoa. [25] Wana wa Yerameeli mzaliwa wa kwanza wa Hesroni walikuwa: Ramu mzaliwa wake wa kwanza, Buna, Oreni, Osemu na Ahiya. [26] Yerameeli alikuwa na mke mwingine, aliyeitwa Atara, aliyekuwa mama yake Onamu. [27] Wana wa Ramu mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli walikuwa: Maasi, Yamini na Ekeri. [28] Wana wa Onamu walikuwa: Shamai na Yada. Wana wa Shamai walikuwa: Nadabu na Abishuri. [29] Mke wa Abishuri aliitwa Abihaili, ambaye alimzalia Abani na Molidi. [30] Wana wa Nadabu walikuwa Seledi na Apaimu, lakini Seledi alikufa bila kuzaa watoto. [31] Apaimu akamzaa: Ishi ambaye alikuwa baba wa Sheshani. Sheshani akamzaa Alai. [32] Wana wa Yada, nduguye Shamai walikuwa: Yetheri na Yonathani. Yetheri alikufa bila kuzaa watoto. [33] Wana wa Yonathani walikuwa: Pelethi na Zaza. Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yerameeli. [34] Sheshani hakuwa na watoto wa kiume, ila wasichana tu. Alikuwa na mtumishi Mmisri aliyeitwa Yarha. [35] Sheshani akamwoza huyu mtumishi wake Yarha binti yake, akamzalia mwana jina lake Atai. [36] Atai akamzaa Nathani, Nathani akamzaa Zabadi, [37] Zabadi akamzaa Eflali, Eflali akamzaa Obedi, [38] Obedi akamzaa Yehu, Yehu akamzaa Azaria, [39] Azaria akamzaa Helesi, Helesi akamzaa Eleasa, [40] Eleasa akamzaa Sismai, Sismai akamzaa Shalumu, [41] Shalumu akamzaa Yekamia, naye Yekamia akamzaa Elishama. [42] Wana wa Kalebu nduguye Yerameeli walikuwa: Mesha mzaliwa wake wa kwanza alimzaa Zifu, naye mwanawe Maresha akamzaa Hebroni. [43] Hebroni alikuwa na wana wanne: Kora, Tapua, Rekemu na Shema. [44] Shema alikuwa baba yake Rahamu na Rahamu alikuwa baba wa Yorkeamu na Rekemu alikuwa baba wa Shamai. [45] Shamai akamzaa Maoni na Maoni akamzaa Beth-Suri. [46] Efa, suria wa Kalebu alikuwa mamaye Harani, Mosa na Gazezi. Harani alikuwa baba wa Gazezi. [47] Wana wa Yadai walikuwa: Regemu, Yothamu, Geshani, Peleti, Efa na Shaafu. [48] Maaka suria wa Kalebu alikuwa mamaye Sheberi na Tirhana. [49] Pia Maaka akamzaa Shaafu babaye Madmana, na Sheva babaye Makbena na Gibea. Kalebu alikuwa na binti jina lake Aksa. [50] Hawa ndio waliokuwa wazao wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa mkuu wao wa Efrathi, walikuwa: Shobali akamzaa Kiriath-Yearimu, [51] Salma akamzaa Bethlehemu, naye Harefu akamzaa Beth-Gaderi. [52] Wazao wa Shobali, baba yake Kiriath-Yearimu, walikuwa: Haroe, nusu ya wakazi wa mji wa Menuhothi, [53] pamoja na koo za Kiriath-Yearimu ambazo ni: Waithiri, Waputhi, Washumathi na Wamishrai. Kutokana na watu hawa walizaliwa Wasorathi na Waeshtaoli. [54] Wazao wa Salma walikuwa: Bethlehemu, Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, nusu ya Wamanahathi, Wasori, [55] pamoja na koo za waandishi zilizoishi katika mji wa Yabesi: yaani Watirathi, Washimeathi na Wasukathi. Hawa ndio Wakeni waliotokana na Hamathi, baba wa nyumba ya Rekabu.
