1 Nyakati 1:1-54 ONEN
[1] Adamu, Sethi, Enoshi, [2] Kenani, Mahalaleli, Yaredi, [3] Enoki, Methusela, Lameki, Noa. [4] Wana wa Noa walikuwa: Shemu, Hamu na Yafethi. [5] Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi. [6] Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma. [7] Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu. [8] Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani. [9] Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani. [10] Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa katika nchi. [11] Misraimu akawazaa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi, [12] Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti) na Wakaftori. [13] Wana wa Kanaani walikuwa: Sidoni, mzaliwa wake wa kwanza, na Hethi, [14] Wayebusi, Waamori, Wagirgashi, [15] Wahivi, Waariki, Wasini, [16] Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. [17] Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu. Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki. [18] Arfaksadi akamzaa Shela, Shela akamzaa Eberi. [19] Eberi alipata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani. [20] Wana wa Yoktani walikuwa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera, [21] Hadoramu, Uzali, Dikla, [22] Obali, Abimaeli, Sheba, [23] Ofiri, Havila na Yobabu. Wote hawa walikuwa wana wa Yoktani. [24] Wana wa Shemu walikuwa Arfaksadi, Shela, [25] Eberi, Pelegi, Reu, [26] Serugi, Nahori, Tera, [27] Tera akamzaa Abramu (yaani, Abrahamu). [28] Abrahamu alikuwa na wana wawili: Isaki na Ishmaeli. [29] Hawa ndio waliokuwa wazao wa Hagari: Nebayothi mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, Kedari, Adbeeli, Mibsamu, [30] Mishma, Duma, Masa, Hadadi, Tema, [31] Yeturi, Nafishi na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli. [32] Wana waliozaliwa na Ketura suria wa Abrahamu walikuwa: Zimrani, Yokshani, Medani, Midiani, Ishbaki na Shua. Wana wa Yokshani walikuwa: Sheba na Dedani. [33] Wana wa Midiani walikuwa: Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Eldaa. Wote hao walikuwa wa uzao wa Ketura. [34] Abrahamu alikuwa baba wa Isaki. Wana wa Isaki walikuwa: Esau na Israeli. [35] Wana wa Esau walikuwa: Elifazi, Reueli, Yeushi, Yalamu na Kora. [36] Wana wa Elifazi walikuwa: Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi; Elifazi kwa Timna akamzaa Amaleki. [37] Wana wa Reueli walikuwa: Nahathi, Zera, Shama na Miza. [38] Wana wa Seiri walikuwa: Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, Dishoni, Eseri na Dishani. [39] Wana wa Lotani walikuwa wawili: Hori na Homamu. Lotani alikuwa na dada yake aliyeitwa Timna. [40] Wana wa Shobali walikuwa: Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu. Wana wa Sibeoni walikuwa: Aiya na Ana. [41] Mwana wa Ana alikuwa: Dishoni. Nao wana wa Dishoni walikuwa: Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani. [42] Wana wa Eseri walikuwa: Bilhani, Zaavani na Akani. Wana wa Dishani walikuwa: Usi na Arani. [43] Hawa ndio wafalme waliotawala Edomu kabla hajatawala mfalme yeyote wa Waisraeli: Bela mwana wa Beori, ambaye mji wake ni Dinhaba. [44] Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake. [45] Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake. [46] Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi. [47] Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake. [48] Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati, akawa mfalme baada yake. [49] Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake. [50] Baal-Hanani alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu. [51] Naye Hadadi pia akafa. Wakuu wa Edomu walikuwa: Timna, Alva, Yethethi, [52] Oholibama, Ela, Pinoni, [53] Kenazi, Temani, Mibsari, [54] Magdieli na Iramu. Hao ndio wakuu wa makabila ya Edomu.
