Yoshua 21:1-45 ONEN
[1] Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli [2] huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “BWANA aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.” [3] Hivyo kama vile BWANA alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe. [4] Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini. [5] Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase. [6] Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani. [7] Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni. [8] Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile BWANA alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose. [9] Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina [10] (miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia): [11] Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.) [12] Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake. [13] Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna, [14] Yatiri, Eshtemoa, [15] Holoni, Debiri, [16] Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili. [17] Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba, [18] Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne. [19] Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho. [20] Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu: [21] Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri, [22] Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne. [23] Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni, [24] Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne [25] Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili. [26] Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki. [27] Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili; [28] kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi, [29] Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne [30] kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni, [31] Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne. [32] Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano. [33] Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho. [34] Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta, [35] Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne; [36] kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa, [37] Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne; [38] kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu, [39] Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne. [40] Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili. [41] Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho. [42] Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote. [43] Kwa hiyo BWANA akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo. [44] BWANA akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, BWANA akawatia adui zao wote mikononi mwao. [45] Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya BWANA kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.
