Mwanzo 10:1-32 ONEN
[1] Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika. [2] Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi. [3] Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma. [4] Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu. [5] (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.) [6] Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani. [7] Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani. [8] Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani. [9] Alikuwa mwindaji hodari mbele za BWANA. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za BWANA.” [10] Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari. [11] Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala, [12] na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa. [13] Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi, [14] Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori. [15] Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi, [16] Wayebusi, Waamori, Wagirgashi, [17] Wahivi, Waariki, Wasini, [18] Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika, [19] na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha. [20] Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao. [21] Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi. [22] Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu. [23] Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki. [24] Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi. [25] Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani. [26] Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera, [27] Hadoramu, Uzali, Dikla, [28] Obali, Abimaeli, Sheba, [29] Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani. [30] Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki. [31] Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao. [32] Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.
