Ezra 2:1-70 ONEN
[1] Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake, [2] wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana): Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa: [3] wazao wa Paroshi 2,172 [4] wazao wa Shefatia 372 [5] wazao wa Ara 775 [6] wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812 [7] wazao wa Elamu 1,254 [8] wazao wa Zatu 945 [9] wazao wa Zakai 760 [10] wazao wa Bani 642 [11] wazao wa Bebai 623 [12] wazao wa Azgadi 1,222 [13] wazao wa Adonikamu 666 [14] wazao wa Bigwai 2,056 [15] wazao wa Adini 454 [16] wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98 [17] wazao wa Besai 323 [18] wazao wa Yora 112 [19] wazao wa Hashumu 223 [20] wazao wa Gibari 95 [21] watu wa Bethlehemu 123 [22] watu wa Netofa 56 [23] watu wa Anathothi 128 [24] watu wa Azmawethi 42 [25] wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743 [26] wazao wa Rama na Geba 621 [27] watu wa Mikmashi 122 [28] watu wa Betheli na Ai 223 [29] wazao wa Nebo 52 [30] wazao wa Magbishi 156 [31] wazao wa Elamu ile ingine 1,254 [32] wazao wa Harimu 320 [33] wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 725 [34] wazao wa Yeriko 345 [35] wazao wa Senaa 3,630 [36] Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973 [37] wazao wa Imeri 1,052 [38] wazao wa Pashuri 1,247 [39] wazao wa Harimu 1,017 [40] Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia) 74 [41] Waimbaji: wazao wa Asafu 128 [42] Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 139 [43] Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi, [44] wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni, [45] wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu, [46] wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani, [47] wazao wa Gideli, Gahari, Reaya, [48] wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu, [49] wazao wa Uza, Pasea, Besai, [50] wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu, [51] wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri, [52] wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha, [53] wazao wa Barkosi, Sisera, Tema, [54] wazao wa Nesia na Hatifa. [55] Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda, [56] wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli, [57] wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami. [58] Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392 [59] Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli: [60] wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 652 [61] Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo). [62] Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi. [63] Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu. [64] Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360; [65] tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200. [66] Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245, [67] ngamia 435 na punda 6,720. [68] Walipofika kwenye nyumba ya BWANA huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake. [69] Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000 za dhahabu, mane 5,000 za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo. [70] Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.
