1 Nyakati 8:1-40 ONEN
[1] Benyamini akamzaa: Bela mzaliwa wake wa kwanza, Ashbeli mwanawe wa pili, Ahara mwanawe wa tatu, [2] Noha mwanawe wa nne na Rafa mwanawe wa tano. [3] Wana wa Bela walikuwa: Adari, Gera, Abihudi, [4] Abishua, Naamani, Ahoa, [5] Gera, Shefufani na Huramu. [6] Hawa ndio wazao wa Ehudi, waliokuwa viongozi wa jamaa za wale walioishi huko Geba na ambao walihamishiwa Manahathi: [7] Naamani, Ahiya na Gera. Gera alikuwa baba yao Uza na Ahihudi na ndiye aliwaongoza kwenda uhamishoni. [8] Shaharaimu aliwazaa wana katika nchi ya Moabu baada ya kuwapa talaka wake zake wawili yaani, Hushimu na Baara. [9] Kwa mkewe Hodeshi, akawazaa wana saba: Yobabu, Sibia, Mesha, Malkamu, [10] Yeuzi, Sakia na Mirma. Hawa ndio waliokuwa wanawe, viongozi wa jamaa zao. [11] Hushimu alimzalia: Abitubu na Elpaali. [12] Wana wa Elpaali walikuwa: Eberi, Mishamu, Shemedi (aliyeijenga miji ya Ono na Lodi, pamoja na vijiji vilivyoizunguka), [13] na Beria na Shema, waliokuwa viongozi wa zile jamaa zilizokuwa zinaishi katika mji wa Aiyaloni, na ambao waliwafukuza wenyeji wa Gathi. [14] Wana wa Beria walikuwa Ahio, Shashaki, Yeremothi, [15] Zebadia, Aradi, Ederi, [16] Mikaeli, Ishpa, na Yoha. [17] Zebadia, Meshulamu, Hizki, Heberi, [18] Ishmerai, Izlia na Yobabu ndio waliokuwa wana wa Elpaali. [19] Yakimu, Zikri, Zabdi, [20] Elienai, Silethai, Elieli, [21] Adaya, Beraya na Shimrathi walikuwa wana wa Shimei. [22] Wana wa Shashaki walikuwa Ishpani, Eberi, Elieli, [23] Abdoni, Zikri, Hanani, [24] Hanania, Elamu, Anthothiya, [25] Ifdeya na Penueli. [26] Shamsherai, Sheharia, Athalia, [27] Yaareshia, Eliya na Zikri walikuwa wana wa Yerohamu. [28] Hawa wote walikuwa viongozi wa jamaa zao wakuu, kama ilivyoorodheshwa katika koo zao, nao waliishi Yerusalemu. [29] Yeieli alikuwa baba yake Gibeoni naye aliishi huko Gibeoni. Mke wake aliitwa Maaka. [30] Mwanawe mzaliwa wa kwanza alikuwa Abdoni, akafuatiwa na Suri, Kishi, Baali, Neri, Nadabu, [31] Gedori, Ahio, Zekeri, [32] na Miklothi ambaye alikuwa baba yake Shimea. Hawa pia waliishi karibu na jamaa zao huko Yerusalemu. [33] Neri akamzaa Kishi, Kishi akamzaa Sauli, Sauli akamzaa Yonathani, Malki-Shua, Abinadabu na Esh-Baali. [34] Yonathani akamzaa: Merib-Baali, naye Merib-Baali akamzaa Mika. [35] Wana wa Mika walikuwa: Pithoni, Meleki, Tarea na Ahazi. [36] Ahazi akamzaa Yehoada. Naye Yehoada akawazaa Alemethi, Azmawethi na Zimri, naye Zimri akamzaa Mosa. [37] Mosa akamzaa Binea, Binea akamzaa Rafa, na mwanawe huyo ni Eleasa, na mwanawe huyo ni Aseli. [38] Aseli alikuwa na wana sita; haya ndiyo majina yao: Azrikamu, Bokeru, Ishmaeli, Shearia, Obadia na Hanani. Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Aseli. [39] Wana wa Esheki, nduguye Aseli, walikuwa: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Ulamu, wa pili Yeushi na wa tatu Elifeleti. [40] Wana wa Ulamu walikuwa mashujaa hodari walioweza kutumia upinde. Alikuwa na wana wengi na wajukuu, jumla yao 150. Hawa wote ndio walikuwa wazao wa Benyamini.
